Timu ya taifa ya vijana ya Rwanda imeanza vibaya mashindano ya dunia ya mchezo wa tennis yanayoendelea nchini Kenya, baada ya kufungwa na Nigeria kwa alama za jumla 3-0.
Rwanda ilishindwa katika mechi 3, moja ikiwa ni kati ya Ernest Habiyambere aliyefungwa na Emmanuel Sylvester kwa seti ya 6-1 na 7-5, lakini pia Joseph Ubon wa Nigeria alimshinda Olivier Haguvimana kwa seti ya 6-0 na 6-1.
Na kwa upande wa wachezaji wawili wawili pia Nigeria iliifunga Rwanda, na katika mashindano hayo katika kanda ya Afrika, Rwanda iko kundi A pamoja na timu za Benin, na Cameroun.
Katika mechi nyingine zilizopigwa jana, wenyeji Kenya wameendeleza wimbi la ushindi kwa kuwafunga Msumbiji kwa alama 3-0 za jumla.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |