Mshambuliaji wa Brazil Neymar jana alilazimika kukatisha mazoezi baada ya kujihisi maumivu ya mguu wakati timu hiyo ikijiaandaa na mechi dhidi ya Costa Rica siku ya Ijumaa.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ambaye amerejea uwanjani baada muda wa miezi mitano aliyokuwa majeruhi, inadaiwa kuwa alichezewa visivyo kwenye mechi dhidi ya Uswisi jumatatu iliyopita.
Wakati huohuo mchezaji wa timu ya Uingereza Dele Alli naye yupo katika hali ya hatihati na huenda akakosa mechi ijayo dhidi ya Panama siku ya jumapili, kutokana na majeruhi ya paja aliyopata kwenye mechi ya kwanza ya timu yake dhidi ya Tunisia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |