Timu ya taifa ya Rwanda imepangwa kundi A pamoja na timu za Canada, Uholanzi na Croatia kwenye mashindano ya dunia ya mchezo wa mpira wa wavu kwa watu wenye ulemavu (sittin volleyball) yatakayofanyika julai 15-22 mwaka huu nchini Uholanzi.
Hii ni mara ya kwanza kushiriki michuano hiyo na walifuzu baada ya kuifunga Misri kwenye mashindano ya Afrika yaliyomalizika mwezi Septemba.
Kati mataifa sita yanayoshiriki michuano hiyo inayohusisha timu za wanaume na wanawake, Rwanda na Misri ndizo timu pekee kutoka Afrika zinazoshiriki.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |