Magoli matatu ya kipindi cha pili yametosha kabisa kupunguza kasi ya Argentina kusonga mbele katika michuano hiyo. Argentina inatakiwa sasa kupata ushindi mnono dhidi ya Nigeria ili kujiweka katika nafasi nzuri kwani hadi sasa anapointi 1 tu.
Mechi iliyopigwa uwanja wa Ekaterinburg baina ya Ufaransa na Peru, imeshuhudia Kylian Mbappe wa Ufaransa akiiweka timu yake kwenye nafasi nzuri ya kwenda hatua ya 16 bora baada ya kufunga goli dakika ya 34 dhidi ya Peru kwenye mchezo wa kundi C.
Nayo Denmark imelazimishwa sare ya goli 1-1 na Australia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |