Rais Xi Jinping wa China amesisitiza umuhimu wa kushikilia mawazo ya ujamaa wenye umaalumu wa China kwenye zama mpya katika kazi za kidiplomasia.
Rais Xi ameyasema hayo kwenye mkutano wa mambo ya kidiplomasia ya kamati kuu ya Chama cha Kikoumunisti cha China. Amesema tangu kufanyika kwa mkutano wa 18 wa kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China, kazi za kidiplomasia zimepiga hatua kubwa.
Aidha, Rais Xi amesema nchi zinazoendelea ni wenzi wa kiasili wa China katika mambo ya kimataifa, China inapaswa kukuza ushirikiano na nchi hizo ili kupata maendeleo ya pamoja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |