Didier Munyaneza mwenye miaka 20 ameshinda taji la mwaka huu la mbio za baiskeli za nchini Rwanda zilizomalizika jana mjini Kigali.
Munyaneza alitumia saa 3 dakika 55 na sekunde 12 kwenye umbali wa kilomita 150 wenye mizunguko 12, akimshinda kwa sekunde 2 tu Mathew Twizerane aliyeshinda nafasi ya pili.
Awali ushindi wa mbio hizo ulitazamiwa kwenda kwa mabingwa wa kimataifa Joseph Areruya na Bonaventure Ewiyezimana ambao nao walishiriki mashindano hayo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |