Ukuaji wa sekta ya viwanda nchini Tanzania unaendlea kuenda chini, jambo ambalo linatingisha uchumi wa nchi.
Ripoti ya Pato la Taifa (GDP) iliyochapishwa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwezi huu inasema uzalishaji wa viwanda ulikua kwa asilimia 7.1 mwaka jana, ikilinganishwa na asilimia 7.8 iliyorekodiwa mwaka 2016.
Bei ya sasa ya soko, ripoti ya hivi karibuni ya Pato la Taifa inaonyesha kwamba thamani ya uzalishaji wa viwanda iliongezeka hadi Sh trilioni 6.41 mwaka jana, kutoka Sh trilioni 5.07 mwaka uliopita.
Baadhi ya wadau wanaamini kuwa tatizo la ukuaji wa chini wa uzalishaji wa viwanda hutokea na kutokuwa na mazingira mazuri ya biashara na soko.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |