• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Ligi Kuu ya Rwanda: Bingwa kupatikana kesho baada ya Mechi za Mwisho kuchezwa

    (GMT+08:00) 2018-06-26 10:34:07

    Ili kutwaa ubingwa ligi kuu, klabu ya APR inapaswa kupata pointi moja tu itakapocheza dhidi ya Espoir FC katika mechi za mwisho za ligi hiyo zitakazopigwa kesho juni 27.

    APR ina pointi 63 na tofauti ya magoli ikiwa ni 35 baada ya kucheza mechi 29, ikifuatiwa na AS Kigali yenye pointi 60 na tofauti ya magoli ikiwa ni 29.

    Kwa hesabu za mpira AS Kigali inaweza kutwaa ubingwa endapo itashinda magoli mengi, na ili iwe hivyo ni lazima APR ipoteze katika mchezo wake.

    APR ni mabingwa wa kihistoria wa ligi soka nchini Rwanda iliyoanzishwa mwaka 1975, kwani wameshinda mara 16.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako