Colombia kupata ushindi wa goli 1-0 lililofungwa na Yerry Mina dakika ya 74, limewafanya Senegal kuaga michuano hiyo licha ya kufanana kila kitu na Japan waliofanikiwa kuingia hatua ya 16 bora.
Japan anafuzu kwa kipengele cha fair play ikiwa na maana kuwa Japan wameoneshwa kadi chache za njano zaidi ya Senegal waliofanana nao kila kitu, hivyo sasa ni wazi timu zote 5 zilizokuwa zinaiwakilisha Afrika zimetolewa katika hatua ya makundi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |