Michuano ya kombe la dunia kwa sasa ipo kwenye mechi za hatua ya mtoano, ambapo katia hatua ya kumi na sita bora inayoendelea hivi sasa, timu za Ufaransa, na Uruguay ziliibuka na ushindi dhidi ya Argentina na Ureno siku ya jumamosi. Nazo Croatia na wenyeji Urusi zikifuzu kwa hatua ya robo fainali baada ya ushindi zilizoupata kwa njia ya penati kila moja dhidi ya Hispania na Denmark mtawalia.
Kwa hiyo, Argentina, Ureno, Hispania na Denmark zimeondolewa kwenye mashindano hayo.
Na hatua hiyo ya kumi na sita bora inaendelea leo kwa mechi mbili, Brazil watacheza dhidi ya Mexico, na Japan watacheza dhidi ya Ubeligiji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |