• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Soka, Kagame Cup: Simba yaishinda APR

    (GMT+08:00) 2018-07-03 10:59:43

    Klabu ya soka ya Simba ya Tanzania jana imepata ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya APR kutoka Rwanda kwenye mechi ya raundi ya pili ya hatua ya makundi katika michuano ya kombe la Cecafa inayoendelea mjini Dar es Salaam.

    Magoli ya simba yalipatikana kupitia, Adam Salamba kunako dakika ya 76, jingine likipatikana katika dakika ya 91 kupitia Meddie Kagere kwa njia ya penati.

    Kwenye mechi hiyo, APR ndiyo walikuwa wa kwanza kupata goli katika kipindi cha kwanza kupitia Nkinzi Fiston.

    Simba sasa inafikisha alama 6 kwenye kundi C sawa Singida united lakini zikitofautiana wingi wa magoli.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako