Waendesha baiskeli 18 wameanza kambi rasmi mjini Musanze kwa ajili ya mashindano ya mbio za baiskeli za kimataifa za Rwanda, Tour Du Rwanda yatakayofanyika rasmi kuanzia Agosti 5 na kumalizika Agosti 12.
Kwa mujibu wa kocha mkuu wa timu ya taifa ya Rwanda yam bio za baiskeli Sterling Magnell, waendesha baiskeli hao watakaa kambini hapo hadi mashindano yatakapoanza.
Katika mashindano haya ambayo ni ya kumi, pamoja na timu tatu kutoka Rwanda pia yatahusisha timu sita mpya za kimataifa kutoka, Algeria, Afrika Kusini, Ufaransa, Ujerumani, na Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |