Kwa sare hiyo, Simba imemaliza na pointi saba, sawa na Singida United, lakini Wekundu wa Msimbazi wanaidadi kubwa ya mabao.
Mechi nyingine za michuano hiyo, APR ya Rwanda imeichapa mabao 4-1 Dakadaha ya Somalia na kumaliza nafasi ya tatu kwenye Kundi C kwa pointi zake tatu.
Nayo Azam fc ya Tanzania wamepata ushindi wa goli 2-1 dhidi ya JKU yas Zanzibar, huku Vipers ya Uganda imeifunga Kator fc ya Sudan Kusini mabao 3-0. Michuano hiyo inaendelea leo kwa mechi kati ya ASPorts ya Djibouti itakutana na Gor Mahia ya Kenya, nayo Lydia Ludic ya Burundi itavaana na Rayon Sports ya Rwanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |