Utafiti wa kamati ya masuala ya fedha ya benki kuu ya Kenya umeonyesha kwamba ushuru wa asilimia 16 wa petroli utachangia mfumko wa uchumi na kupanda kwa gharama ya maisha.
Ushuru huo mpya utakaoanza kutumika mwezi Septemba mwaka huu utaathiri sekta ya viwanda,uchukuzi,kilimo na kawi.
Wataalamu wa fedha wanasisitiza kwamba bei ya bidhaa za msingi zinatarajiwa kupanda katika mda wa miezi ijayo.
Shirika la kitaifa la takwimu limeangazia kikwazo hicho kuzuia ukuwaji wa asilimia 5.7 mwaka huu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |