Ikicheza mechi yake ya kundi B, Gor Mahia ya Kenya imeifunga AS Ports ya Djibouti kwa mabao 2-0 na kumaliza jinamizi la sare lililokuwa likiwaandama.
Kwenye mchezo mwingine uliochezwa Chamazi, Rayon Sports ya Rwanda imeisambaratisha Lydia Ludic ya Burundi kwa goli 3-1.
Timu 8 zimefuzu hatua ya robo fainali ya michuano hii kutoka kundi A ni Azam fc ya Tanzania, Vipers ya Uganda na JKU ya Zanzibar. Kundi B, ni Rayon Sports ya Rwanda, Gor Mahia ya Kenya na AS Ports ya Djibouti. Na kundi C zipo Simba na Singida United za Tanzania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |