• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mechi ya kwanza ya Robo fainali kupigwa leo

    (GMT+08:00) 2018-07-06 08:32:57

    Siku ya leo kutakuwa na mechi ya kwanza ya robo fainali kati ya Uruguay na Ufaransa. Mchezo huo utachezwa kwenye uwanja wa Nizhny Novgorod majira ya saa 11 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.

    Timu zote mbili zipo kwenye vuwango bora, lakini Uruguay ambao ni mabingwa wa kombe la dunia mwaka 1930 na 1950 wanaonekana kuwa na rekodi nzuri zaidi baada ya kushinda mechi zote kwenye hatua ya makundi, huku Ufaransa mabingwa wa mwaka 1998, wakishinda mechi mbili na kutoka sare moja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako