Toleo la kichina na kiingereza la kitabu cha kwanza cha kielektroniki cha "Rais Xi Jinping azungumzia utawala wa nchi" kilichochapishwa na shirika la uchapishaji la lugha za kigeni la China limetolewa leo ili kufahamisha jumuiya ya kimataifa kuhusu wazo la Ujamaa wenye sifa ya China katika zama mpya la Xi Jinping..
Maudhui yaliyomo kwenye kitabu hicho cha kielektroniki kilichotolewa kwenye majukwaa manne ya biashara za kidigitali ikiwemo Amazon na Overdrive, yatawasaidia wasomaji wa nchi mbalimbali duniani kufahamu kwa kasi na urahisi wazo la Ujamaa wenye sifa maalum ya China katika zama mpya la Xi Jinping.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |