Waziri mkuu wa China Li Keqiang amesema kuwa hakuna atakayenufaika katika vita ya kibiashara, lakini China itachukua hatua za kujibu kama jambo hilo likitokea.
Li Keqiang amesema hayo alipokutana na waandishi wa habari mjini Sofia, Bulgaria, akiwa na mwenyeji wake Boyko Borissov.
Waziri mkuu wa China yuko nchini Bulgaria kwa ziara ya kikazi, na pia kuhudhuria mkutano wa 7 wa China na nchi 16 za Katikati na Mashariki mwa Ulaya.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |