TIMU ya JKT Queens imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara kwa kishindo, baada ya kumaliza na pointi 42 na ikiwa imeshinda mechi zake zote 14.
Katika mechi yake ya mwisho iliyopigwa jana dhidi ya mabingwa watetezi wa ligi hiyo Mlandizi Queens, JKT ilishinda kwa magoli 6-2.
Kigoma Sisters imemaliza katika nafasi ya pili kwa pointi zake 30, ikifuatiwa na Alliance Girls yenye pointi 24 na nafasi ya nne imekwenda kwa Mlandizi Queens walioambulia pointi 22.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |