Ripoti zinadai kuwa Mshambuliaji wa kimataifa wa Ureno Cristiano Ronaldo ametua rasmi katika klabu ya Juventus ya Italia kwa mkataba wa miaka minne kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni 99.5, na atakuwa akilipwa mshahara wa pauni milioni 26.5 kwa mwaka.
Klabu ya Real Madrid jana imetoa taarifa ya kumshukuru mchezaji huyo miaka 33 kwa mafanikio makubwa aliyoiletea katika kipindi cha misimu tisa ya soka aliyocheza pale Santiago Bernabeu na akitajwa kuwa kuandika historia kubwa ya klabu katika zama alizocheza.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |