Bibi Hua amesema China itachukua hatua ya kulinda maslahi yake halali, na kwamba vita ya kibiashara iliyoanzishwa na Marekani ni vita kati ya upande mmoja na pande nyingi, ni vita kati ya kitendo cha kujilinda kibiashara na biashara huria, na pia ni vita kati ya umwamba na utaratibu. Amesema China itashirikiana na jumuiya ya kimataifa kulinda utaratibu wa biashara wa pande nyingi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |