• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Russia yasema ukosoaji wa Trump dhidi ya mradi wa gesi kati ya Russia na Ujerumani unalenga kuhimiza uuzaji wa gesi ya Marekani

    (GMT+08:00) 2018-07-13 08:59:16

    Msemaji wa Ikulu ya Russia Bw. Dmitry Peskov amesema ukosoaji wa rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya mradi wa bomba la gesi kati ya Russia na Ujerumani, unalenga kuhimiza uuzaji wa gesi ya Marekani iliyosindikwa LNG kwa Ulaya. Bw. Peskov ameitaja kauli hiyo ya Trump kuwa ni tangazo la ushindani usio wa haki, na kusema bei ya gesi ya LNG ya Marekani itakuwa juu zaidi kuliko gesi ya Russia kupitia bomba. Msemaji huyo pia amesema mradi huo hautaifanya Ujerumani ambayo ni mteja mkubwa wa gesi ya Russia, kuitegemea Russia, na kinyume chake utakuwa uhakikisho wa utoaji gesi wenye uhakika, na kuhimiza maendeleo ya kunufaishana kati ya nchi hizo mbili kwenye nyanja mbalimbali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako