Shirikisho la soka Kenya (FKF), imetuma rasmi malalamiko kwa shirikisho la soka Afrika (CAF), dhidi ya timu ya taifa ya wanawake ya Equatoria Guinea, ikilalamikia kitendo cha taifa hilo kutumia mamluki wakati wa mchezo baina ya timu hzio mbili hivi karibuni.
Kenya na Equatorial Guinea zilikutana katika mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu fainali za kombe la mataifa ya Afrika kwa wanawake (AFCON 2018), katika mchezo uliopigwa Juni 6 uwanja wa Kenyatta mjini Machakos, Harambee Starlet ilishinda 2-1.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |