Luca Modric wa Croatia ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa michuano ya kombe la dunia mwaka 2018, na tuzo ya mchezaji bora mwenye umri mdogo (Chipukizi) imechukuliwa na Kylian Mbappe wa Ufaransa aliyeweka rekodi nyingi kwenye michuano hiyo kutokana na kipaji chake ikiwemo kufunga goli katika mechi ya fainali akiwa na umri mdogo chini ya miaka 20.
Tuzo ya golikipa bora ilichukuliwa na Thibaut Coutois wa Ubeligiji, na mfungaji bora akitangazwa Harry Kane wa Uingereza aliyepachika jumla ya magoli 6.
Lakini timu iliyotangazwa na kupata tuzo ya kuonyesha mchezo wa uungwana michezoni wakati wa michuano hiyo ni Hispania.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |