Licha ya kufuatiliwa na mamilioni ya watu kote duniani kwa njia ya runinga, sherehe za ufungaji michuano ya kombe la dunia mwaka 2018, pamoja na mechi ya fainali, baadhi ya viongozi mashuhuri dunia walihudhuria shughuli hizo za jana zilizofanyika kwenye uwanja wa Luzhniki mjini Moscow.
Wakiongozwa na Rais wa FIFA Gianni Infantino, miongoni viongozi waliyohudhuria ni mwenyeji wa waandaaji wa michuano hiyo, Rais wa Urusi Vladmir Putin, Rais wa Croatia Kolinda Grabar Kitarović, na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron na wote kwa pamoja walikuwa wageni muhimu kwenye shughuli hizo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |