• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tennis: Djokovic ashinda taji la Ubingwa wa Wimbledon

    (GMT+08:00) 2018-07-16 10:47:06

    Novak Djokovic wa Serbia ametwaa ubingwa wa Tennis wa michuano ya Wimbledon baada ya kushinda mechi ya fainali dhidi ya Kevin Anderson wa Afrika Kusini iliyopigwa jana mjini London.

    Djokovic alishinda kwa seti ya 6-2 6-2 na 7-6, na huu unakuwa ubingwa wake wa nne wa michuano ya Wimbledon akiwa amewahi kushinda mwaka tena mwaka 2011, 2014 na 2015.

    Ubingwa huu unakuwa ni wa kwanza tangu apumzike kucheza mwaka 2016 kutokana na majeruhi aliyokuwa nayo.

    Kwa upande wa wanawake, Angelique Kerber wa Ujerumani alishinda taji la Wimbledon kwa kumfunga Serena Williams wa Marekani kwa seti ya alama 6-3 6-3 kwenye mechi ya fainali siku ya jumamosi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako