Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying amekanusha lawama zilizotolewa na Marekani kwenye "Taarifa ya Uchunguzi wa Kipengele cha 301" kwamba China imekuwa ikifanya biashara isiyo na usawa, na kusema, lawama hizo hazina msingi wowote.
Wakati huohuo, Gazeti la FT la Uingereza limetoa makala ikisema, pendekezo la "Ukanda Mmoja na Njia Moja" limekumbwa na matatizo duniani kutokana na hali isiyo na uwazi ya ukusanyaji wa fedha wa China.
Bibi Hua amesema, msimamo huo hauendani na hali hasili, huku akisisitiza kuwa kati ya wenzi wa ushirikiano wa China, bado hakuna nchi yoyote inayokabiliwa na msukosuko wa madeni kutokana na ushirikiano huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |