China na Umoja wa Ulaya zimekubaliana kushirikiana pamoja kulinda kanuni za mfumo wa kimataifa, kuboresha biashara huru na ya pande nyingi.
Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa mkutano wa 20 wa viongozi, ulioendeshwa kwa pamoja na waziri mkuu wa China Li Keqiang, mwenyekiti wa Baraza la Ulaya Donald Tusk, na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulaya Jean-Claude Juncker.
Taarifa iliyotolewa baada ya mkutano huo imesema, China na Umoja wa Ulaya zina wajibu wa pamoja wa kulinda kanuni za mfumo wa kimataifa, kutetea pande nyingi, kuunga mkono biashara huria, na kuboresha amani, utulivu na maendeleo ya dunia katika hali ya sasa ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |