• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IMF ladumisha makadirio ya ongezeko la uchumi, laonya kuongezeka mivutano ya kibiashara

    (GMT+08:00) 2018-07-17 09:14:39

    Shirika la Fedha la kimataifa IMF limedumisha makadirio ya ongezeko la uchumi kwa mwaka huu na mwaka kesho, lakini limetahadharisha kuhusu kuongezeka kwa mivutano ya biashara inayoweza kuuyumbisha ufufukaji wa uchumi wa dunia.

    Kwenye ripoti iliyopitiwa upya kuhusu mwenendo wa uchumi wa dunia na kutolewa jana, IMF imesema mwaka huu na mwaka kesho ongezeko la uchumi wa dunia linatarajiwa kufikia asilimia 3.9, kama ilivyokadiriwa mwezi Aprili.

    Hata hivyo IMF imesema makadirio hayo yanaweza kupungua kutokana na kuongezeka kwa mivutano ya kibiashara kati ya Marekani na washirika wake wa biashara. Ripoti imesema ushuru mpya uliotangazwa na Marekani na ushuru wa kulipiza kisasi uliotangazwa na washirika wake wa biashara umeongeza uwezekano wa kuongezeka kwa mivutano ya kibiashara.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako