Shirikisho la mchezo wa mpira wa Wavu la Rwanda limeiandikia barua wizara ya michezo ya nchi hiyo, ya kuomba ruhusa kwa ajili ya timu ya taifa ya wanawake ya kwenda kushiriki mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 20 yaakayofanyika nchini Kenya kuanzia Agosti 24 hadi Septemba 3 mwaka huu.
Akitibisha kuandika barua, katibu mkuu wa shirikisho hilo Adarlbert Mfashimana, amewaambia waandishi wa habari kuwa, mchakato wa maandalizi kwa ajili ya timu hiyo umekamilika na kwamba timu hiyo kwa sasa iko katika hali nzuri ya kiushindani, na sasa wanasubiri majibu ya Wizara kuhusu hatma ya timu kwenda au kutokwenda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |