Tanzania imepata mkopo wa zaidi ya dola milioni 400 kutoka kwa benki ya biashara na Maendeleo za kufadhili mradi wa reli ya kisasa na kiwanda kuzalisha megawati 318 kutokana na gesi.
Hii inakuwa ni mara ya kwanza kwa serikali kutafuta mkopo, hapo awali Rais John Magufuli alikuwa amesema serikali ina pesa za kutosha kufadhili mradi wa reli hiyo utakaogharimu dola bilioni 2.5.
Miezi mitatu iliopita Tanzania ilikopa fedha zingine kufadhili mradi wake wa kuzalisha megawati 2,100 wa Stieglers Gorg
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |