Wakulima wa mpunga katika tarafa ya Pawaga na Idodi Wilaya ya Iringa vijijini wanakabiliwa na ukosefu wa mashine za kisasa za kuvuni, jambo linalosababisha zao kupotelea shambani wakati wa uvunaji.
Walizungumza hayo wakati wa ziara ya mwakilishi kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO) nchini, Fredy Kafeero yenye lengo kukagua miradi inayofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU).
Mwenyekiti wa skimu ya umwagiliaji Mkombozi, Salehe Mohammed alisema miundombinu ya kuvunia ni duni, vifaa hakuna hivyo wanalazimika kufyeka na kusababisha mpunga kupotolea shambani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |