Ushindi huo wa Gor Mahia unawafanya waendelee kukalia nafasi ya pili katika kundi D wakifikisha jumla ya alama 5 huku MC Alger walio kileleni wakiwa na pointi 7 wakati Rayon Sports ya Rwanda ikishika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 2.
Yanga imekuwa timu ya kwanza ndani ya kundi hilo kuruhusu mabao 9 baada ya kipigo cha mabao 4-0 dhidi ya MC Algeria kwenye mchezo wa kwanza uliopigwa huko Algeria.
Mchezo mwingine: mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Thomas Ulimwengu, ameifungia bao la ushindi El Hilal ikiibwaga Songo ya Msumbiji magoli 2-1 katika mchezo wa Kundi B uwanja wa Al Hilal mjini Omdurman.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |