Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania (Kilimanjaro Queens) inatarajia kucheza mchezo wa kwanza dhidi ya wenyeji Rwanda, huku Kenya inakutana uso kwa uso na Uganda.
Timu zitakazoshiriki kwenye michuano hiyo ni wenyeji Rwanda, Ethiopia, Uganda, Kenya na Tanzania.
Rais wa pili wa shirikisho la soka la Rwanda (FERWAFA) Bwana Habyarimana Marcel amesema kuwa maandalizi ya michuano hiyo yamekamilika na kuwataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kuangalia burudani bora ya soka la wanawake.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |