• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Usain Bolt kufanyiwa majaribio ligi ya Australia

    (GMT+08:00) 2018-07-19 08:33:13

    Bingwa mara nane wa Olimpiki Usain Bolt ameanza mazungumzo kwa ajili ya majaribio ya kusakata soka nchini Australia.

    Mwanariadha huyo raia wa Jamaica mwenye umri wa miaka 31, anafanya mazungumzo ya kusaini kandarasi ya wiki sita na klabu ya Central Coast Mariners, klabu inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini humo.

    Afisa mkuu wa klabu ya Mariners Shaun Mielekamp amesema kuwa klabu hiyo ilitumia miezi minne kumsaka Bolt na mkataba wa muda mrefu huenda ukafuata baadaye.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako