• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • FIBA yawafungia wachezaji na kocha kutokana na ugomvi

    (GMT+08:00) 2018-07-20 08:19:03
    Shirikisho la mchezo wa kikapu Dunia (FIBA) jana limetangaza kuwafungia maisha wachezaji 13 na kocha baada ya kuzuka kwa ugomvi katika mchezo wa kufuzu fainali za Dunia za mchezo wa kikapu kwa upande wa bara la Asia kati ya Ufilipino na Australia.

    FIBA imewafungia wachezaji 10 wa Ufilipino kutocheza michezo 35 huku wachezaji watatu wa Australia wakifungiwa jumla ya michezo tisa. Kocha wa Ufilipino Vincent Reyes amesimamishwa mchezo mmoja.

    Vyama vya mchezo wa kikapu vya nchi zote pia vimetozwa faini na kuamriwa mchezo ujao wa nyumbani kucheza bila ya mashabiki.

    Ugomvi huo katika robo ya tatu ya mchezo ambao Australia ilishinda kwa alama 89-53 ambapo wachezaji zaidi ya tisa wa timu mwenyeji waliingia uwanjani na kuzua ugomvi ambao ulichukua dakika 30 kuamuliwa kabla ya kuendelea tena.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako