• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Gor Mahia wapata ushindi kwenye 'Mashemeji Derby'

    (GMT+08:00) 2018-07-23 11:17:14

    Gor Mahia wamefanikiwa kuibuka na ushindi muhimu wa magoli 2-1 kwenye mechi ya kutaka na shoka, dhidi ya mahasimu wao wa kihistoria katika soka la Kenya, timu ya AFC Leopards iliyopigwa kwenye uwanja wa Moi mjini Nairobi.

    Gor ilipata golila kwanza kupitia Jacques Tuyisenge katika dakika ya 21, baadaye dakika chache kuelekea mapumziko Leopards walisawazisha kupitia Whyvonne Isuza, lakini bahati ikarejea kwa Gor baada ya George Odhiambo kufunga goli la pili na likiwa ni la ushindi katika dakika ya 53.

    Kwa ushindi huu Gor wanafikisha pointi 52 katika nafasi ya kwanza kwenye msimamo wa ligi kuu nchini Kenya na wakiwa ni timu pekee amabyo haijafungwa kwenye ligi hiyo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako