Idara kuu ya ushuru wa forodha ya China leo imesema, kampuni za China zimezingatia zaidi kulinda hakimiliki ya kiujuzi kuliko zamani.
Takwimu mpya zilizotolewa na idara hiyo zinaonesha kuwa, katika nusu ya kwanza ya mwaka huu, kampuni 871 za China zimetoa maombi ya kuhifadhi hakimiliki ya kiujuzi, na kesi 2,796 zimepitishwa na idara hiyo.
Aidha, idara hiyo imesema China itaongeza adhabu kali kwa vitendo vya kukiuka sheria ya kulinda hakimiliki ya kiujuzi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |