Shirika la haki za binadamu nchini Syria limesema waasi na wanafamilia wao 900 wameondoka mkoa wa Daraa ulioko kusini mwa Syria katika saa 24 zilizopita, ikiwa ni sehemu ya makubaliano yanayoungwa mkono na Russia, ambayo yanaruhusu waasi na raia wasiotaka kuafikiana na serikali kuondoka mkoa huo na kwenda maeneo yanayodhibitiwa na waasi kaskazini mwa Syria. Jeshi la Syria limetwaa asilimia 90 ya mkoa wa Daraa kupitia operesheni za kijeshi au maafikiano ya kisiasa tangu Juni 19.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |