• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • CECAFA Wanawake 2018: Tanzania na Ethiopia Zapata ushindi

    (GMT+08:00) 2018-07-24 10:29:35

    Timu za taifa za Tanzania na Ethiopia jana zimepata ushindi kwenye mechi zake za jana kwenye mashindano ya kombe la CECAFA kwa wanawake.

    Kwenye mechi ya kwanza, Tanzania ilipata ushindi wa magoli 4-1 dhidi ya Uganda na kuifanya timu hiyo ifikishe pointi 4 kwenye kundi, na magoli hayo yakifungwa na Donisia Daniel, Asha Hamza na nahodha Asha Rashid aliyefunga mawili, huku bao pekee la Uganda likifungwa na Shadya Nankya.

    Nayo Ethiopia ilipata ushindi mnono wa magoli 3-0 dhidi ya wenyeji Rwanda katika mechi ya pili, na Katika mechi zijazo za timu hizo, Tanzania inatarajiwa kucheza na Ethiopia siku ya ijumaa, lakini kabla ya hapo Ethiopia itacheza mechi moja dhidi ya Kenya jumatano.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako