Makamu mwenyekiti wa kamati ya Olimpiki na Michezo ya Rwanda, Bi. Felicite Rwemalika amepitishwa kuwa miongoni mwa wagombea wa nafasi ya ujumbe wa kamati ya kimataifa ya Olimpiki katika uchaguzi mkuu utakaofanyika kwenye mkutano mkuu utakaofanyika Oktoba 8 na Oktoba 9 mwaka huu mjini Buenos Aires nchini Argentina.
Bi. Rwemalika anaungana William Blick kutoka Uganda, kuwa viongozi pekee wa nchi za Afrika Mashariki wanaowania nafasi hizo.
Mwishoni mwa juma lililopita, Kamati ya maadili ya IOC iliendesha uchunguzi dhidi ya mienendo ya Rwemalika na Blick, na kuwaona kuwa wanafaa kuwania nafasi tisa za ujumbe wa IOC ambazo ziko wazi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |