Senegal imechaguliwa kuwa mwandaaji wa hafla ya Tuzo ya CAF ya mchezaji Bora wa Afrika kwa mwaka 2018 zitakazofanyika Januari 9 mwaka 2019.
Rais wa shirikisho la mpira wa miguu la Senegal Augustin Senghor amethibitisha kupokea wito wa kuwa mwenyekiti wa maandalizi ya shughuli hiyo.
Naye Rais wa Senegal Macky Sally ambaye mwaka jana alipokea tuzo ya heshima ya CAF kutokana na juhudi zake kuendeleza soka, amedai kupokea taarifa hiyo kwa furaha na kuruhusu mji wa Dakar kuwa mwenyeji.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |