Rais alipokea gawio hilo jijini Dar es Salaam kutoka kwa kampuni na mashirika hayo, ambayo serikali ina hisa zake au inamiliki kwa asilimia 100 alisema, fedha hizo zinatarajiwa kuwezesha serikali kuendelea kutekeleza miradi yake ya maendeleo na kuboresha huduma mbalimbali za jamii.
Magufuli alimuagiza Msajili wa Hazina, Athuman Mbuttuka, kuhakikisha mashirika yote yanatoa gawio kwa serikali, na yatakayoshindwa uongozi wake ubadilishwe au mashirika hayo yafutwe.
Alisema katika miaka miwili gawio limeongezeka, lakini kiasi kinachopatikana bado ni kidogo sana ikilinganishwa na uwekezaji uliofanyika.
Serikali iliwekeza zaidi ya Sh trilioni 49.05 kwenye taasisi na kampuni mbalimbali, lakini baadhi ya mashirika hayajakabidhi mgao wao kwa serikali.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |