• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Mauzo ya Kenya Uingereza yapungua

    (GMT+08:00) 2018-07-24 19:23:15
    Ripoti ya taasisi ya maendeleo ODI imesema kwamba mauzo ya bidhaa za Kenya kwenye soko la Uingereza yamepungua ikilinganishwa nan chi nyingine zinazoshindania soko hilo.

    Aidha, taakwimu kutoka kwa kituo cha kimataifa cha biashara zinaonyesha kuwa mauzo ya Kenya kwenye soko la Uingereza yamepungua kutoka shilingi bilioni 50 mwaka 2009 hadi bilioni 37 mwaka 2017.

    Taasisi hiyo imesema mauzo kwenye soko hilo kutoka kote duniani yameongezeka kwa asilimia 15 mwaka 2017.

    Mwaka huo wa 2017 kenye ilikuwa imepoteza mgao wake wa soko la Uingereza wa bidhaa zake tatu kuu kwa nchinyingine.

    Mkuu wa utafiti kwenye shirika la maendeleo ya kiuchumi Dirk Wellem Te Velde amesema Kenya imepoteza ushindani wake na hivyo inahitaji kuongeza kampeni za kukuza tena mauzo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako