• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Eritrea na Ethiopia kucheza mechi ya kihistoria mwezi Agosti

    (GMT+08:00) 2018-07-25 09:08:31

    Kwa mara ya kwanza katika historia ya soka, nchi za Eritrea na Ethiopia zinatarajiwa kucheza mechi ya kirafiki mwishoni mwa mwezi Agosti mwaka huu ikiwa ni sehemu ya mwendelezo wa makubaliano ya amani yaliyosainiwa na viongozi wa mataifa hayo mawili yaliyokuwa kwenye vita kali kwa kipindi cha miaka 20.

    Mechi hiyo inatarajiwa kuchezwa mjini Asmara nchini Eritrea kwa ridhaa ya pande zote mbili, na hii ni baada ya viongozi wa nchi Abiy Ahmed wa Ethiopia na Isaias Afwerki wa Eritrea kusaini makubaliano ya amani Julai 9 mwaka huu, na kila moja kufanya ziara kwa mwenzake ndani ya kipindi cha wiki moja tu.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako