Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI UNAIDS limezitaka nchi kuchukua hatua zenye nguvu katika kutatua msukosuko wa kujikinga na UKIMWI kwenye Mkutano wa 22 wa Kimataifa wa UKIMWI mjini Amsterdam, Uholanzi.
Shirika hilo limesema watu takriban milioni 1.8 waliambukizwa virusi vya UKIMWI mwaka jana na nchi zipatazo 50 zimeshuhudia ongezeko la maambukizi mapya ya UKIMWI, ambapo huduma za kujikinga na UKIMWI hazitolewi kwa wigo na ufanisi wa kutosha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |