• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya-Wakulima wa parachichi watafuta soko China na India,baada ya bei ulaya kuporomoka

    (GMT+08:00) 2018-07-25 19:35:11

    Wakulima wa parachichi nchini Kenya wamelekeza macho yao nchini China na India kutafuta bei nzuri ya zao hilo kufuatia ushindani mkubwa katika soko la muungano wa nchi za ulaya.

    Bei za parachichi ulaya zimeshuka kwa zaidi ya nusu kutokana na kuongezeka kwa bidhaa hiyo haswa kutoka Peru na Afrika Kusini.

    Mfuko wa kilo nne wa parachichi ulizwa kwa kati ya Sh471.88 na Sh589.85 (€4 and €5) ikilinganishwa na bei ya kati ya Sh1,297.67 — Sh1, 533.61) mwaka jana.

    Afisa Mkuu Mtendaji wa Chama cha Wazalishaji Mazao Safi Okisegere Ojepat amesema bei hizo za chini zimewaumiza wakulima kwa sababu mvua iliyonyesha kwa kipindi kirefu ilifanya zao hilo kuchelewa kukomaa na hatimaye kuvuna sawa na wakulima wa Peru.

    Akizungumza kwa njia ya simu Ojepat alisema sasa wanatafuta masoko mapya katika Mashariki ya mbali.Alielezea imani yake kwamba China na India zitafungua milango.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako