Gazeti la Sueddeutsche Zeitung la Ujerumani limeeleza uamuzi wa mchezaji huyo kuwa ni kipigo kamili cha majira ya joto, wakati mtaalamu maarufu wa soka la Ujerumani Raphael Honingstein ameandika kuhusiana na kujiuzulu Oezil kutoka katika timu ya taifa kuwa ni hali mbaya kuliko kushindwa kokote katika kombe la dunia.
Naye kansela wa Ujerumani Angela Merkel amemshukuru Mesut Oezil kwa mchango wake katika timu ya hiyo ya taifa ya Ujerumani.
Kiungo huyo amestaafu soka ya kimataifa akilalamikia kufanyiwa ubaguzi na chama cha soka Ujerumani baada ya kutolewa mbuzi wa kafara baada ya timu hiyo kutolewa mapema kwenye fainali za michuano ya kombe la dunia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |