• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya:Tullo yasitisha oparesheni kwa ukosefu wa usalama

    (GMT+08:00) 2018-07-26 19:40:44

    Kampuni ya kuchimba mafuta katika eneo la Turkana nchini Kenya Tullow Oil imesitisha shughuli zake kwa wiki 2 kufuatia ukosefu wa usalama wa kutosha katika eneo hilo.

    Kwa mujibu wa afisa mkuu wa kampuni hiyo, Paul McDade amesema maandamano ya wakaazi wakitaka manufaa ya moja kwa moja ya asilimia 5 ya mradi huo katika eneo hilo yametia hofu kazi zao .

    Hata hivyo, ameahidi kwamba wataendelea na oparesheni zao pindi tu tatizo hilo litakaposuluhishwa.

    Tullow inalenga kufikisha mapipa laki moja ya mafuta kwa siku kufikia mwaka 2021 -22.

    Kwa sasa inasafirisha mapipa 600 kila siku hadi katika bandari ya Mombasa swala ambalo wanakijiji wameanza kulipinga kwa kudai fedha.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako