• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Uganda:Serikali kudhibiti mauzo ya nje ya sukari

    (GMT+08:00) 2018-07-26 19:41:02
    Serikali ya Uganda imeamua kudhibiti mauzo ya sukari nje ya nchi na inataka kusitisha kamwe biashara hiyo ili kuimarisha soko la ndani.

    Maamuzi haya yanajiri baada ya kushuhudiwa kwa kasoro ya sukari nchini Kenya iliyochangia wafanyibiashara kukimbilia soko hilo.

    Hatua hiyo sasa imechangia kuongezeka kwa bei ya sukari nchini Uganda kwani sukari nyingi imeishilia Kenya.

    David Kiiza afisa katika wizara ya biashara Uganda amesema watahakikisha marufuku hayo yanatekelezwa kwani zaidi ya tani elfu 25 za sukari zimeuzwa nje ya nchi .

    Amesisitiza kwamba wataruhusu tani elfu 10 pekee za sukari kuuzwa nje .

    Upande mwengine wafanyibiashara wa sukari wamejitetea wakisema Uganda ina sukari ya kutosha na uuzaji wa sukari nchini Kenya hautaathiri bidhaa hiyo sokoni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako